Mafunzo ya Mtaala mpya wa Umahiri ngazi ya Sekondari yameanza Kisiwani Pemba.

Mkurugenzi Mtendaji Taasisi ya Elimu ya Zanzibar Nd. Abdalla Mohammed Mussa amewataka walimu kuwatayari kuufanyia kazi Mtaala mpya wa Sekondari ambao unakusudia Kuwawezesha wanafunzi kuwa na ujuzi na utambuzi wa fursa zilizomo kwenye jamii. Akifungua mafunzo ya siku nne kwa wakufunzi wa walimu (TOT) huko katika Kituo cha walimu Michakaini kisiwani Pemba amesema katika utekelezaji wa Mtaala huo ni lazima walimu kuwa na utayari kwani wao ndio watekelezaji wakubwa wa mtaala huo wanaotegemewa katika kuwaandaa wanafunzi darasani. Aidha amewataka Wakufunzi wa walimu wanaopatiwa mafunzo hayo kwenda kuwafahamisha walimu kuwa Mabadiliko ya Mtaala ni jambo la kawaida kulingana na mahitaji ya jamii husika pamoja na Mabadiliko ya sayansi na teknolojia. Amesema Mafunzo hayo yatawasaidia walimu katika kuutumia Mtaala mpya wa umahiri kwa Ngazi ya Sekondari. Akiwasilisha Mada ya Utelezaji wa Mtaala Ulioboreshwa kwa ngazi ya Sekondari Muwezeshaji Kutoka Taasisisi ya Elimu Tanzania Hwago Hassan Hwago amesema Elimu ya Sekondari sasa itakua na mikondo miwili ambayo ni mikondo wa Jumla na Mkondo wa Amali. Ameeleza kuwa Mtaala mpya wa Sekondari umetoa fursa kwa wanafunzi kujifunza Elimu ya Amali ili kuwawezesha wanafunzi hao kujiajiri wanapomaliza masomo yao.

Huduma Tunazotoa

Huduma zinazotolewa na Taasisi ya Elimu ya Zanzibar.

Mitaala

Kuishauri Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar juu ya mambo yanayohusiana na ukuzaji Mitaala ya Elimu ya Maandalizi, Msingi, Elimu ya Sekondari pamoja na Vyuo vya Ualimu

Tafiti

Kufanya tafiti za Elimu na Kuthibiti Ubora kwenye vifaa vya kufundishia na kujifunzia

Vifaa vya Kufundishia

Kuratibu Utayarishaji wa Vifaa vya Kufundishia na Kujifunzia kwa walimu na wanafunzi

Kutoa Mafunzo

Kutoa Mafunzo kazini yanayohusiana na Mitaala na Vifaa vya Kufundishia na Kujifunzia

Viongozi Wetu

23Miaka

Ya uzoefu katika kutoa huduma ya Mitaala

6657Walimu

Jumla ya walimu waliopatiwa
mafunzo ya mitaala

7760Walimu

Tunategemea kuwapatia mafunzo
ya Mtaala mpya 2024

1,222,756
Vitabu vya Mwalimu na Mwanafunzi

Vimeshapishwa kwa ajili
ya mtaala mpya 2024