- Mkutano wa mwaka wa Jukwaa la Viongozi wa Elimu ya Sekondari
- Mafunzo ya Mfumo wa Masjala (e-office)
- Uzinduzi wa programu 10 za Redio za kujifunza lugha ya Kiingereza
- Muendelezo wa Utoaji wa Mafunzo kwa Walimu
- Muendelezo wa Utoaji wa Mafunzo kwa Walimu - Pemba
- Utiaji saini Mkataba wa Uchapishaji Vitabu kwaajili ya Skuli binafsi Zanzibar
- Kikao cha kutathmini utekelezaji wa Mradi wa Elimu Mjumuisho Zanzibar
- Mafunzo ya Utekelezaji wa Mtaala mpya kwa Walimu wa Maandalizi na Msingi wanaofundisha watoto wenye Mahitaji Maalumu ya kielimu.
- Mafunzo ya Mtaala mpya kwa Walimu wanaofundisha watoto wenye Mahitaji Maalumu
- Kikao kazi cha Kubadilishana Uzoefu katika Masuala ya Elimu ya Watu Wazima
- Ziara ya Kujenga Uhusiano mwema
- Mjumbe wa Sekretarieti ya GPE Lucinda Ramos ametembelea TEZ
- TEZ yapokea Ugeni kutoka Gambia
- TEZ yafanya Mkutano na Walimu wakuu wa Skuli za Sekondari Pemba
- TEZ na TET kuandaa muongozo wa kutolea mafunzo ya utekelezaji wa Mtaala mpya kwa walimu wa Sekondari.
- UDOM na TEZ kukusanya maoni ili kutengeza Moduli mpya za mafunzo ya walimu wa Msingi na Sekondari.
- WEMA Kupokea Ripoti ya upembuzi yakinifu (needs assessement report) ya Upitiaji wa Mitaala ya Mafunzo ya Ualimu.
Pata matukio mapya nahabari mbali mbali kutoka zie.

Mahafali ya Skuli ya High Achievement
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Elimu ya Zanzibar Abdalla Mohamed Musaa akiwakabidhi vyeti wanafunzi walio maliza ngazi ya Maandalizi na Msingi katika Mahafali ya Skuli ya High Achievement Iliyopo Mbweni Matrekta. Mahafali hayo yamefanyika katika ukumbi wa hoteli ya Verde Mkoa wa Mjini Magharibi. Akizungumza na walimu pamoja na wazazi wa wanafunzi wa skuli hiyo Nd. Abdalla amewapaongeza walimu kwa juhudi kubwa wanazochukua kuwajenga wanafunzi katika malezi Bora. Aidha amewasisitiza kuutumia vyema Mtaala mpya wa Umahiri ambao umekusudia kuwajenga wanafunzi kivitendo. Sambamba na hayo amewataka wazazi wa wanafunzi kufatilia maendeleo ya wanafunzi pamoja na kuwa karibu nao ili kuwalinda na vitendo vya udhalilishaji.